Video News4 videos from 3 sources
Rais William Ruto ametia saini mswada wa Marekebisho ya Ushuru wa Thamani (VAT) unaopunguza ushuru wa mafuta kutoka asilimia 16 hadi 8 kwa muda wa miezi mitatu. Hii ni baada ya serikali kutafuta msaada wa dharura kutoka Benki ya Dunia kukabiliana na gharama ya juu ya mafuta. Hata hivyo, wakazi wa Makueni wamesema bei mpya za mafuta bado hazijapunguza makali ya gharama ya maisha. Mbali na hayo, Mstaafu Jaji Mkuu David Maraga amekashifu ufisadi katika mpango wa uagizaji mafuta kati ya Kenya na mataifa ya Kiarabu.
KTN News (Youtube)









